IQNA

Uungaji mkono wa vyuo vikuu vya Qur'ani kwa wananchi wa Gaza

8:23 - December 31, 2008
Habari ID: 1725222
Vyuo vya mafunzo ya Qur'ani nchini Iran vimetangaza wazi uungaji mkono wao kwa wananchi wa Palestina na hasa wa Ukanda wa Gaza wanaodhulumiwa na utawala ghasibu wa Israel na kusisitiza kwamba viko tayari kutekeleza amri ya Kiongozi Mudhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran katika kuwatetea wananchi hao wanaoteseka na kukandamizwa na Wazayuni.
Vyuo hivyo vimetoa taarifa vikitangaza kwamba, kutokana na mauaji ya umati yanayofanywa na utawala ghasibu wa Israel dhidi ya wanawake na watoto wasio na hatia wa Gaza, pamoja na hatua yake ya kulipua ovyo makazi ya raia, misikiti na vituo vya kielimu vya Gaza na hasa Chuo cha Kiislamu cha eneo hilo, wanachuo na wahadhiri wa vyuo hivyo kote nchini Iran wako tayari kutekeleza amri yoyote itakayotolewa na Kiongozi Muadhamu kuhusiana na jinai hizo za utawala wa Kizayuni.
Taarifa hiyo imesema kuwa, wanachuo na wafanyakazi wa vyuo hivyo vya Qur'an sambamba na Waislamu wa maeneo mengine ya dunia, wameshiriki kwa wingi katika maandamano makubwa ya kulaani jinai hizo ambazo zinatekelezwa na Wazayuni huku ulimwengu unaodai kuwa umestaarabika na kutetea haki za binadamu, ukiwa umeketi kimya bila kuchukua hatua yoyote ya maana katika kuzua mauaji yanayofanywa na utawala huo dhidi ya raia wasio na hatia wa Palestina.
Taarifa hiyo pia imebainisha hasira na masikitiko makubwa kutokana na kimya na hata ushirikiano wa baadhi ya watawala wa Kiarabu na utawala wa Tel Aviv katika kuwakandamiza na kuwaua kwa umati Wapalestina wa Ukanda wa Gaza. 340918
captcha