Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA katika mji wa Qum kusini mwa Tehran, kongamano hilo litajadili mapambano ya fakhari ya wapigania ukombozi wa Palestina na namna walivyoathiriwa na Mapinduzi ya Kiisalmu nchini Iran.
Kongamano hilo litahutubiwa na Mkuu wa Idara ya Utamaduni na wanachuo wa kidini kutoka Pakistan, Hujattul Islam Raisi, na Imam wa Ijumaa wa mji wa Ahwaz kusini mwa Iran Hujjatul Islam Hujjati ambaye pia ni mkuu wa Chuo Kikuu cha Kidini cha Khuzestan.
Kongamano hilo litafanyika baada ya swala za Magharibi na Isha'a katika Chuo Kikuu cha Imam Khomeini MA. 359509