Harakati ya Kimataifa ya Kutetea Haki za Watoto, imetoa taarifa ikielezea wasiwasi wake mkubwa na wakati huohuo kukosoa vikali hatua ya utawala haramu wa Israel za kushinikiza, kuzingira na hata kuwakamata watoto wadogo huko katika Ukanda wa Gaza na Ufukwe wa Magharibi wa Mto Jordan katika kipindi cha miezi miwili iliyopita.
Taarifa ya harakati hiyo iliyosomwa katika televisheni ya al-Alam, inasema kuwa idadi ya watoto walio na umri wa miaka 12 na 13 wanaokamatwa katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan imeongezeka sana katika kipindi cha miezi miwili iliyopita. Imesema mwanzoni mwa mwaka huu wa 2009 idadi ya watoto waliokuwa wakishikiliwa katika jela za Wazayuni ilikuwa ni 423, wengi wao wakiwa ni wale waliotiwa mbaroni mwanzoni mwa mapambano ya Intifadha.
Harakati hiyo inasema kuwa hadi sasa utawala huo umewatia mbaroni zaidi ya watoto 6700 wa Kipalestina na kwamba 423 wangali wanateseka katika jela za utawala huo. 397710