IQNA

Hassan as-Swaffar: Maisha ya Ayatullah Bahjat yalijaa zuhdi na irfan

11:08 - May 19, 2009
Habari ID: 1780344
Ofisi ya Sheikh Hassan as-Swaffar, mwanazuoni mashuhuri wa Kishia nchini Saudi Arabia ambaye pia ni Imam wa Ijumaa wa mji wa Qatif jana Jumatatu ilitoa taarifa ikiwatumia salamu za rambirambi wananchi wa Iran na umma mzima wa Kiislamu kwa mnasaba wa kuaga dunia Ayatullahil Udhma Muhammad Taqi Bahjat, mwanazuoni mkubwa wa Kiislamu.
Kwa mujibu wa tovuti ya mwanazuoni huyo wa Saudi Arabia, Hassan Swaffar amesema katika barua yake ya rambirambi kwamba, Ayatullahil Udhma Bahjat aliutumia umri wake wote kwa ajili ya kuihudumia dini tukufu ya Kiislamu. Amesema mwanazuoni huyo alikuwa na sifa zenye thamani kubwa za irfani, jambo ambalo lililonekana wazi katika uso wake. Amesema, mwenendo wake ulibaini wazi kiwango kikubwa cha irfani, unyenyekevu na uchaji Mungu aliokuwa nao. Sheikh Hassan as-Swaffar amesema kuwa kifo cha Ayatullah Bahjat ni msiba mkubwa kwa ulimwengu wa Kiislamu na kutoa mkono wa pole na rambirambi kwa wapenzi wote wa masuala ya kidini na kimaanawi duniani. 407013
captcha