IQNA

Filamu ya Imam Hussein (AS) kutengenezwa Iraq

11:54 - May 21, 2009
Habari ID: 1781119
Watengeneza filamu nchini Iraq wametangaza kuwa watatengeneza filamu kuhusu Mjukuu wa Mtume (SAW), Imam Hussein (AS).
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, mtengeneza filamu Muraqi ajulikanaye kama Qasim ambaye filamu aliyotengeneza hivi karibuni, Al Mughni, imekamilika nchini Ufaransa, amesema sasa yuko tayari kutengeneza filamu kuhusu Imam Hussein (AS) katika mji wa Basra kusini mwa Iraq.
Amesema filamu hiyo itatengenezwa kwa ushirikiano na wawekezaji wa kigeni na kuongeza kuwa atashirikiana na watengeneza filamu wa Syria na Misri katika kazi yake hiyo. 408411
captcha