Tuzo hiyo imetolewa kwa kutambua mchango wao wa kipekee katika nyanja za seli za jua za perovskite, teknolojia ya kugundua seli adimu kwa kutumia microfluidics, na algorithimu za grafu za kiwango kikubwa.
Katika hafla iliyofanyika tarehe 8 Septemba katika Ukumbi wa Vahdat mjini Tehran, maafisa wa serikali, wasomi, na wanasayansi kutoka ulimwengu wa Kiislamu walikusanyika kwa heshima ya washindi wa Tuzo ya Mustafa (SAW) ya mwaka huu.
Tuzo hizo zilitangazwa rasmi na Mahdi Safarinia, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Mustafa, ambaye pia ni Katibu wa Kamati ya Sera ya Tuzo hiyo. Hotuba ya utangulizi ilitolewa na Profesa Ali Akbar Salehi, Mwenyekiti wa Kamati ya Kisayansi ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Mkuu wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran.
Kuhusu Washindi
Mchakato wa Uchaguzi
Katika hafla ya kufunga, Profesa Salehi alieleza mchakato wa uteuzi: kuanzia tangazo la kuwaalia wasomi wawasilishe kazi zao mwezi Februari 2024, kupokea zaidi ya mapendekezo 5,200 katika makundi matatu, hadi orodha fupi ya wagombea 24 waliopitiwa na jopo la wanasayansi 100 wa kimataifa, na hatimaye kuchaguliwa washindi watatu.
Aidha, alitangaza kuwa kwa mara ya kwanza, Medali ya Mwanasayansi Chipukizi imetolewa kwa watafiti watatu kutoka Iran, Malaysia, na Uturuki, ishara ya kuongezeka kwa msisitizo wa tuzo hiyo katika kukuza vipaji vipya.
Kuhusu Tuzo ya Mustafa (SAW)
Tuzo ya Mustafa (SAW), ambayo imepewa jina Mtume Muhamamd Al Mustafa (SAW), ni tuzo ya sayansi na teknolojia inayotolewa kila baada ya miaka miwili na Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Mustafa chini ya mwavuli wa Shirika la Ushirikiano wa Kiislamu (OIC). Lengo lake ni kutambua mafanikio ya kisayansi yenye athari kwa jamii kutoka ulimwengu wa Kiislamu.
Washindi hupokea zawadi ya fedha, medali, na diploma. Tuzo hii inajumuisha makundi kama vile Sayansi na Teknolojia ya Mawasiliano na Habari; Sayansi ya Maisha na Tiba; Sayansi ya Msingi na Uhandisi; na Sayansi ya Nano na Teknolojia ya Nano. Wanaostahiki ni wanasayansi wa imani yoyote wanaofanya kazi katika nchi za Kiislamu, pamoja na Waislamu popote walipo duniani.
Tuzo ya Sayansi ya Mustafa SAW (The Mustafa (PBUH) Prize) ilizinduliwa mwaka 2013 na kisha ilitolewa mara ya kwanza mwaka 2015 mjini Tehran ambapo wakati huo washindi walikuwa ni Profesa Omar Yaghi wa Jordan, mtaalamu wa nanoteknolojia na Profesa Jackie Ying wa Singapore katika uga wa bio-nanoteknolojia.
Tuzo hiyo hutolewa kila baada ya miaka miwili sambamba na maadhimisho ya Maulid ya Mtume Muhammad Al Mustafa (SAW).
3494533