IQNA

Mwezi wa Ramadhani ni fursa ya Umoja wa Waislamu

11:57 - August 17, 2010
Habari ID: 1975094
Kwa kuzingatia mafundisho ya Qur'ani yanayohimiza juu ya kufungamana na kamba ya Mwenyezi Mungu, mazingira ya kimaanawi ya mwezi mtukufu wa Ramadhani ni fursa nzuri ya kuimarisha umoja wa Waislamu kote duniani hasa kati ya viongozi wa mfumo wa Kiislamu wa Iran.
Hayo yamesemwa na Ayatullah Hadavi Tehrani Mkuu wa Taasisi ya Rawaq Hekmat katika mahojiano na IQNA. Mwanazuoni huo maarufu wa Iran amesema katika mwezi mtukufu wa Ramadhani nyoyo za waumini huwa tayari kwa ajili ya ibada na ucha Mungu na kuongoza kuwa katika mwezi huu wenye baraka, Waislamu wanapaswa kuongeza uzingatiwaji wa Qur'ani Tukufu. Amesema hali ya kimaanawi ya mwezi mtukufu wa Ramadhani inaandaa mazingira yanayowapa Waislamu hisia ya kuwa wote wana lengo moja.
634209
captcha