IQNA

Kutuzwa washindi wa mashindano ya Qur'ani ya al-Jabir nchini Imarati

11:37 - August 19, 2010
Habari ID: 1976771
Sherehe ya kushukuriwa na kutuzwa washindi wa mashindano ya 10 ya Qur'ani ya al-Jabir katika Umoja wa Falame za Kirabu ilifanyika siku ya Jumanne huko Abu Dhabi mji mkuu wa Imarati.
Hayo yameripotiwa na gazeti la Imarati la al-Khaleej ambalo limesema kuwa washindi wa mashindano hayo yaliyofanyika katika makundi mawili ya wanawake na wanaume walishukuriwa na kupewa zawadi nono.
Akizungumza katika shehere hiyo, Nassir Hamdan az-Zaabi, mkuu wa Baraza la Uendeshaji wa Kituo cha Qur'ani cha Abu Dhabi ambaye pia ni mkuu wa Baraza la Wadhamini wa Zawadi ya al-Jabir amesema kuwa mashindano hayo hufanyika kila mwaka na kusimamiwa na Idara Kuu ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu ya Imarati. Ameongeza kuwa kwa ujumla, washiriki 105 walishiriki katika mashindano hayo ambapo 53 walikuwa ni wanaume na 53 wanawake, walioshindana katika marhala tofauti za kuhifadhi Qur'ani. 636191
captcha