Kwa mujibu wa gazeti la Imarati la Al Itihad, kongamano hilo ambalo litafanyika kwa mwaka wa pili sasa litawajumuisha wanakaligrafia bora 30 kutoka nchi za Kiislamu na kila mmoja wao ataandika Juzuu moja ya Qur'ani kwa kaligrafia.
Kongamano hili linafanyika kwa himaya ya Wizara ya Utamaduni, Vijana na Ustawi ya Umoja wa Falme za Kiarabu.
Katika kongamano sawa na hili la mwaka jana wanakaligrafia wa Qur'ani kutoka maeneo yote ya ulimwengu wa Kiislamu waliandika msahafu kamili kwa mbinu bora zaidi za kaligrafia. 639926