Kwa mujibu wa shirika rasmi la habari la Saudi Arabia SPA mashindano hayo yanafanyika kwa uungaji mkono wa Rais Zeinul Abideen bin Ali wa Tunisia kwa ajili ya mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Mashindano hayo ambayo yanazishirikisha nchi 21 za Kiislamu na Kiarabu yamefunguliwa na Abubakr al-Akhdhuri, Waziri wa Masuala ya Kidini wa Tunisia. Washindi wa mashindano hayo ya siku kumi watatuzwa na kupewa zawadi baada ya kumalizika rasmi mashindano hayo. 643700