Akizungmza mjini Tehran alipokutana na maafisa wa ngazi za juu wa Harakati ya Amal ya Lebanon, Rais Ahmadinejad ameongeza kuwa wale wanaopambana dhidi ya maadui wa mwanaadamu na madola ya istikbari wana jukumu zito la pamoja. Rais wa Iran ameashiria mwamko katika ulimwengu wa Kiislamu na kusema mfumo wa kibepari na kibeberu duniani umefika ukingoni na kwamba sasa dunia ina kiu ya utawala adilifu.
644882