IQNA

Nuskha ya Qur'ani ya miaka 300 katika maonyesho Ujerumani

11:40 - September 05, 2010
Habari ID: 1987393
Nuskha ya Qur'ani Tukufu iliyoandikwa miaka 300 iliyopita huko India imewekwa katika maonyesho nchini Ujerumani.
Kwa mujibu wa gazeti la Gulf News nuskha hiyo ya Qur'ani yenye upana wa sentimita 14.5 na urefu wa sentimita 24 iliandikwa kwa mkono katika zama za silsili ya Gurkani wakati wa utawala wa serikali ya Aurungzeb mwana wa Shah Jahan ambaye alikuwa muasisi wa jengo maarufu la Taj Mahal.
Kurasa za msahafu huo zimetengenezwa kwa mpunga na mada zinginezo pamoja na kuandikwa kwa wino wa madini yenye thamani.
Imearifiwa kuwa msahafu huo uliandikwa na Aurangzeb na kwamba wakati wa kuandika aliuweka katika eneo maalumu la kasri.
647412
captcha