IQNA

Maonyesho ya Kaligrafia ya Kiislamu yafanyika Pakistan

11:27 - September 07, 2010
Habari ID: 1989142
Maonyesho ya kila mwaka ya kaligrafia ya Kiislamu chini ya anwani ya "Maonyesho ya Kitaifa ya Kaligrafia ya Kiislamu Mwaka 2010" yanafanyika nchini Pakistan katika ukumbi wa Kitaifa wa Sanaa mjini Islamabad.
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, maonyesho hayo yaliyoanza Septemba Mosi yameandaliwa na Baraza la Kitaifa la Sanaa la Pakistan kwa kushirikiana na Wizara ya Utamaduni nchini humo.
Lengo la maonyesho hayo limetajwa kuwa ni kuarifisha thamani za kimaanawi za Uislamu, kuhimiza sanaa ya kaligrafia ya Kiislamu na kuwasaidia waliokumbwa na maafa ya mafuriko nchini Pakistan.
Maonyesho hayo yana athari 150 za wanakaligrafia Waislamu 70 na yanajumuisha kaligrafia ya aya za Qur'ani Tukufu, majina ya Mwenyezi Mungu (Asmaul Husna), jina la Mtume Muhammad (SAW) n.k.
649523


captcha