Mbunge Ed Husic ambaye wazazi wake walihamia nchini Australia miaka mingi iliyopita aligombea na kushinda kiti cha ubunge kwa tiketi ya Leba katika uchaguzi uliofanyika mwezi uliopita.
Alisema katika kampeni za uchaguzi huo kwamba anajivunia kuwa Muislamu na kuchukua hatua ya kuapishwa kwa Qur'ani kabla ya kuanza kuhudumia rasmi bunge la nchi hiyo.
Kabla ya hapo Ed Husic alikuwa kiongozi wa jumuiya moja ya wafanyakazi magharibi mwa mji wa Sydney.
Waislamu wanaunda karibu asilimia 2 ya wakazi wote milioni 22 wa Australia. 665367