Mkusanyiko huo umetayarishwa na Baraza la Makanisa ya Minnesota.
Wafuasi wa dini mbalimbali waliokutana katika mkusanyiko huo wametangaza upinzani wao dhidi ya hujuma ya hivi karibuni dhidi ya Uislamu nchini Marekani na wakaomba dua ya kuenea hali ya kuheshimiana kati ya wafuasi wa dini mbalimbali.
Kiongozi wa Waislamu wa Minnesota Ja'far Siddiqi alihutubia mkusanyiko huo akisema kuwa Waislamu laki moja na nusu wa mji huo wameathiriwa mno na kitendo cha kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu.
Ameongeza kuwa mahudhurio ya wafuasi wa dini mbalimbali katika mkusanyiko huo pamoja na Waislamu yanawapa Waislamu nguvu zaidi na kukabiliana na hujuma zinazolenga matukufu ya dini yao. 665632