IQNA

Iran kushiriki maonyesho ya vitabu Tanzania

14:03 - November 06, 2010
Habari ID: 2026305
Idara ya Utamaduni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Tanzania imetangaza kuwa itaonyesha vitabu vya kidini, kijamii na kiutamaduni katika Maonyesho ya 19 Kimataifa ya Vitabu mjini Dar-es-Salaam.
Maonyesho hayo yametayarishwa na Chama cha Wachapishaji wa Vitabu Tanzania (PATA) kwa ushirikiano wa Baraza la Maendeleo ya Vitabu Tanzania” (BAMVITA).
Maonyesho hayo yametayarishwa kwa lengo la kustawisha utamaduni wa kusoma vitabu katika jamii. Wachapishwaji Tanzania, wawakilishi wa nchi kadhaa za Afrika Mashariki na wachapisaji wa kimataifa watashiriki katika maonyesho hayo.
Idara ya Utamaduni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imepanga kuonyesha vitabu vya kidini na kijamii, majarida na vile vile CD/DVD kwa lugha za Kiarabu, Kiswahili na Kiingereza.
688873
captcha