IQNA

Maktaba yenye nakala adimu za Qur'ani yafunguliwa Imarati

17:18 - November 08, 2010
Habari ID: 2028029
Maktaba ya Turathi za Vitavu vya Kiislamu ya Abu Dhabi ambayo ina nakala adimu za Qur'ani Tukufu zenye umri wa miaka 500 ilifunguliwa jana katika msikiti wa Sheikh Zayid.
Ali Tamim Mwenyekiti wa Baraza la Idara la Msikiti wa Sheikh Zayid amesema kuwa nakala hizo za Qur'ani tukufu zina umri wa miaka 500 na zilitawanywa barani Ulaya kati ya mwaka 1537 na 1857 Miladia.
Amesema kuwa maktaba hiyo ina nakala zenye thamani kubwa za Qur'ani zilizoandikwa kwa hati za mkono, vitabu adimu na nyaraka zenye thamani kubwa. Ameongeza kuwa vitabu vya maktaba hiyo vinahusu maudhui mbalimbali za kisayansi na kiutamaduni na vimeandikwa kwa lugha 12 za dunia. 691061

captcha