IQNA

Kongamano la kumuenzi Sheikhul Ishraq kufanyika Syria

9:21 - December 02, 2010
Habari ID: 2040925
Kongamano la kumuenzi Sheikhul Ishraq litafanyika mapema mwakani nchini Syria kwa hima ya Chuo Kikuu cha Tehran na Taasisi ya Utafiti wa Kifalsafa ya Iran.
Kituo cha habari cha Chuo Kikuu cha Tehran kimeripoti kuwa kongamano hilo linafanyika kwa kutilia maanani nafasi aali ya Sheikh Shahabuddin Yahya Suhrawardi mbaye ndiye muasisi wa Falsafa ya Ishraq (falsafa ya mnururisho) katika ulimwengu wa Kiislamu.
Kwa mujibu wa kituo hicho, kongamano hilo litasimamiwa na Chuo Kikuu cha Tehran na Taasisi ya Utafiti wa Falsafa ya Iran kwa ushirikiano wa Chuo Kikuu cha Damascus na Chuo Kikuu cha Halab kuanzia tarehe 22 hadi 24 Februari. 704518
captcha