IQNA

Vyombo vya habari vitumiwe kukabiliana na chuki dhidi ya Uislamu

18:57 - December 08, 2010
Habari ID: 2044796
Waziri Mkuu wa Malaysia Datuk Seri Najib Tun Razak ametoa wito kwa Waislamu kutumia vyombo vya habari kuwafahmisha walimwengu kuhusu Uislamu halisi ambao ni maridadi na unavutia.
Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Malaysia la Bernama, Waziri Mkuu Najib amesema kuna makundi ambayo yamefanikiwa kutumia vyombo vya habari kwa makusudi na mpangilio maalumu kueneza propaganda chafu dhidi ya Uislamu.
"Tatizo hilo ni sugu hasa wakati propaganda zinapofanikiwa na watu wanaanza kuuchukia Uislamu. Hali hii ya kusikitisha inatokana na Waislamu kushindwa kutumia vyombo vya habari kusahihisha taswira potofu inayoenezwa kuhusu Uislamu", amesema Waziri Mkuu wa Malaysia wakati wa kuzinduliwa Televisheni ya kwanza ya Kiislamu ya nchi hiyo, TV Al Hijrah' mjini Kuala Lumpur.
Najib ameongeza kuwa ni Waislamu wachache wanaomiliki vyombo vya habari na kwamba ukosefu wa ubunifu katika kanali za televisheni za Kiislamu ni jambo ambalo limefanya kizazi cha vijana kutozitazama.
708916

captcha