IQNA

Vitabu vya Shariati vyauzwa kwa wingi katika maonyesho ya Lebanon

13:00 - December 23, 2010
Habari ID: 2052033
Majmui kamili ya vitabu vya marehemu Dakta Ali Shariati kwa lugha ya Kiarabu ni moja ya vitabu vilivyouzwa kwa wingi katika maonyesho ya kimataifa ya vitabu ya Beirut Lebanon kwa kuchukua nafasi ya pili ya mauzo makubwa zaidi ya vitabu katika maonyesho hayo.
Kwa mujibu wa gazeti la kieneo la Dar al-Hayaat, majmui ya vitabu hivyo vilivyochapishwa na taasisi ya Dar al-Amir ya Lebanon imechukua nafasi ya pili ya mauzo mengi ya vitabu vya kidini.
Kitabu cha Swiraat al-Mustaqeem cha Abdallah al-Harari kilichochapishwa na taasisi ya Dar a-Mashaari' ya Lebanon ndicho kitabu kilichochukua nafasi ya kwanza katika sekta hiyo ya mauzo ya vitabi vya kidini.
Duru ya 54 ya maonyesho hayo ya kimataifa ya vitabu yaliyoyashirikisha mashirika mbalimbali ya uandishi na uchapishaji vitabu ikiwemo Taasisi ya Fikra ya Kiislamu na Taasisi ya al-Huda ya Uchapishaji wa Kimataifa inayofungamana na Taasisi ya Utamaduni na Uhusiano wa Kiislamu ya Iran ilifanyika mjini Beirut tokea tarehe 6 hadi 16 Disemba. Zaidi ya mashirika 200 ya Lebanon, nchi za Kiarabu na kimataifa yalishiriki kwenye maonyesho hayo. 716849
captcha