IQNA

Kikao cha Sira ya Mtume SAW kufanyika Mash'had

12:56 - December 29, 2010
Habari ID: 2055502
Kikao cha sita katika mfululizo wa vikao kuhusu Sira ya Mtume SAW kimepangwa kufanyika katika Chuo cha Kidini cha Narjes katika mji mtakatifu wa Mash'had kaskazini mashariki mwa Iran.
Mkuu wa Masuala ya Utamaduni katika Vyuo Vikuu vya Kidini Mkoani Khorassan Hujjatul Islam Muhammad Ramadhani amemwambia mwandishi wa IQNA kuwa kikao hicho kutahudhuriwa na Ayatullah Ayazi mwanazuoni mwandamizi katika Vyuo Vikuu vya Kidini vya Khorassan. Atatoa hotuba kuhusu maadili katika maisha ya Mtume SAW.
Kikao hicho kimeandaliwa kwa ajili ya wanachuo wa kike kutoka vyuo vya kidini vya Esmatia, Bibi Khadija na Bibi Zahra katika mkoa huo.
Idara ya Utamaduni katika vyuo vya kidini vya Khorassan imekuwa ikiandaa semina za mara kwa mara kuhusu sira ya Mtume SAW tokea mwanzo wa mwaka huu.
720068
captcha