IQNA

Uharibiwaji wa maeneo ya Wapalestina waongezeka kwa asilimia 38

16:54 - January 29, 2011
Habari ID: 2071948
Kwa mujibu wa takwimu za hivi karibuni za Kituo cha Kiarabu cha Mipango Mbadala ACAP, uharibiwaji wa maneo ya Wapalestina unaofanywa na utawala haramu wa Israel uliongezeka kwa asilimia 38 mwaka uliopita wa 2010 licha ya kuwepo upinzani mkubwa wa jamii ya kimataifa dhidi ya jambo hilo.
Kwa mujibu wa kituo kilichotajwa utawala wa Kizayuni tokea mwaka 2009 hadi 2010 ulibomoa nyumba 227 za Wapalestina katika ardhi unazozikalia kwa mabavu tokea mwaka 1984.
Nyumba za Wapalestina katika vijiji vya jangwa la Naqab ambavyo havijawahi kutambuliwa rasmi na utawala huo ni miongoni mwa maeneo ya Wapalestina yaliyoharibiwa na utawala huo.
Utawala huo umekuwa ukidumisha siasa za kiuadui dhidi ya Wapalestina kwa kuharibu kwa makusudi nyumba zao na kuwafukuza kutoka kwenye ardhi zao za jadi huku jamii ya kimataifa ikiendelea kunyamazia kimya unyama huo. 738087
captcha