IQNA

Masomo ya Qur'ani kutolewa katika Akademia ya Sayansi za Kiislamu Australia

12:06 - February 03, 2011
Habari ID: 2074610
Masomo ya muda ya Qur'ani Tukufu yataanza kutolewa katika Akademia ya Uhakiki na Sayansi za Qur'ani (ISRA) katika mji wa Sydney nchin Autralia kwa kipindi cha wiki 30.
Tovuti ya Muslim Villae imeripoti kuwa masomo hayo yataanza tarehe 12 Februari. Mpango huo ni sehemu ya masomo yanayotolewa na akademia hiyo kwa shabaha ya kutoa mafunzo ya tajwidi na mbinu za kiraa ya Qur'ani Tukufu.
Masomo hayo yanafundisha mbinu za kisasa za kiraa ya Qur'ani Tukufu na watakaofaulu watapewa shahada za kiraa na tajwidi ya Qur'ani. 740714
captcha