Kwa mujibu wa tovuti ya tradearabia.com kikao hicho kilichoandaliwa na Jumuiya ya Kimataifa ya Uchumi wa Kiislamu kilihudhuriwa pia na balozi wa Malaysia nchini Bahrain Bwana Sayyid Sultan Idris.
Jamil al-Jarudi, Mkurugenzi Mwandamizi wa Benki ya Elaf ambaye alikuwa mgeni wa heshima amezungumzia mustakbali wa biashara na uchumi wa Kiislamu na pia changamoto zinazoukabili. Vilevile wataalamu wa masuala ya kiuchumi walioshiriki kwenye kikao hicho wamechunguza suala hilo kwa kina.
Njadala kuhusu uoni mpana wa biashara na uwekezaji wa Kiislamu katika dunia ya leo ni lengo kuu la kufanyika kikao hicho. 745346