IQNA

Kongamano la Umoja wa Kiislamu Tehran kujadili matukio ya ulimwengu wa Kiislamu

16:41 - February 14, 2011
Habari ID: 2080910
Karibu wasomi 250 mashuhuri wa Kiislamu kutoka nchi 57 wanatazamiwa kuhudhuria Kongamano la 24 la Kimataifa la Umoja wa Kiislamu mjini Tehran kuanzia Februari 19-21 ambapo suala la matukio ya hivi karibuni katika ulimwengu wa Kiislamu litapewa umuhimu.
Katibu Mkuu wa Taasisi ya Kimataifa ya Kukurubisha Pamoja Madhehebu ya Kiislamu Ayatullah Muhammad Ali Taskhiri amesema kuwa kongamano hilo la Umoja wa Kiislamu litakalofanyika mjini Tehran litaangazia pia mikakati ya kuimarisha ukuruba wa madhehebu ya Kiislamu.
Akihutubia kikao cha waandishi habari Februari 13, Ayatullah Taskhiri ameashiria matukio ya kihistoria katika nchi kadhaa za Kiarabu na kusema kuwa kongamano lijalo la umoja wa Kiislamu litaangazia kwa kiwango kikubwa matukio hayo.
Aidha amesema kongamano la mwaka huu litatathmini makongamano 20 yaliyopita ya Umoja wa Kiislamu.
Kati ya watakaohudhuria kongamano hilo ni Rais Mahmoud Ahmadinejad wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran atakayehutubu katika kikao cha ufunguzi na Dkt. Sayyed Mohammad Husseini Waziri wa Utamaduni na Muongozo wa Kiislamu.
746919
captcha