Akihutubia umati mkubwa wa Waislamu wakati wa Sala ya Ijumaa kwenye uwanja wa Chuo Kikuu cha Tehran, Ayatullah Kashani amelikosoa Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi kwa misimamo yake ya kindumakuwili kuhusu mwamko unaoshuhudiwa katika eneo hili. Amesema kwa upande mmoja baraza hilo limetangaza kuwaunga mkono wananchi wa Syria na Libya na kwa upande mwingine limefumbia macho jinai wanazofanyiwa wananchi wa Bahrain na Yemen wanaoandamana kupinga tawala za kiimla katika nchi hizo. Amesisitiza kuwa Mashariki ya Kati mpya inaelekea kuzaliwa na hakuna mtu yeyote anayeweza kuzima ari ya wananchi wa eneo hili ya kutaka usawa na uadilifu kwenye safu ya uongozi.
778672