Jumatano iliyopita mawaziri wa utawala wa Kizayuni wa Israel walisherehekea ufunguzi wa nyumba 1,000 za walowezi wa Kiyahudi katika mtaa wa Kipalestina wa Ras al Amud katika eneo la Mlima wa Zeitun mjini Quds.
Taasisi ya Waqfu na Turathi ya Al Aqsa imetoa taarifa na kusema utawala wa Kizayuni unapanga kujenga nyumba zaidi za walowezi wa Kiyahudi katika eneo hilo. Taarifa hiyo imesema kitongoji kipya kinachopanga kujengwa hapo kutakuwa na daraja itakayounganishwa na Msikiti wa Al Aqsa.
Taasisi ya Waqfu na Turathi ya Al Aqsa imeonya kuwa utawala wa Kizayuni umetoa wito kwa Mayahudi kuhamia katika kitongoji hicho kwa sababu kiko karibu na Al Aqsa.
Viongozi wa Palestina wametoa wito kwa nchi za Kiislamu duniani kuchukua hatua za kivitendo kukabiliana na njama za Wazayuni za kuharibu Msikiti wa Al Aqsa ambao ndio kibla cha kwanza cha Waislamu.
798401