IQNA

Msaada wa kifedha wa Banki ya Kiislamu ya Abu Dhabi kwa mipango ya msalaba mwekundu

17:59 - June 01, 2011
Habari ID: 2132503
Banki ya Kiislamu ya Abu Dhabi ADIB ya nchini Imarati imetiliana saini hati ya maelewano na Shirika la Msalaba Mwekundu kwa ajili ya kuunga mkono kifedha shirika hilo katika mipango yake ya kutoa masomo kwa wanafunzi.
Kwa mujibu wa tovuti ya Zawya benki hiyo ya Kiislamu imeahidi kushirikiana na shirika hilo la Msalaba Mwekundu kwa madhumuni ya kuimarisha thamani na malengo ya kiutu pamoja na kukidhi mahitaji ya kijamii.
Kwa mujibu wa mapatano yaliyofikiwa, benki hiyo itakuwa ikidhamini gharama za masomo kwa wanafunzi ambao wazazi wao hawana uwezo wa kuwalipia karo za shule na wale walio na hamu ya kunufaika na masomo yanayotolewa katika vituo maalumu vya masomo ya kitaalamu. 802694
captcha