IQNA

Harakati za kimapinduzi za Imam Khomeini ni ilhamu kwa muamko wa Kiislamu duniani

10:22 - June 05, 2011
Habari ID: 2133187
Khatibu wa muda wa Sala ya Ijumaa hapa jijini Tehran amesema leo kuwa harakati za kimapinduzi zilizofanywa na Imam Sayyid Ruhullah Khomeini zaidi ya miongo mitatu iliyopita zimechochea muamko unaoonekana hivi sasa katika ulimwengu wa Kiislamu.
Hujjatul-Islam Sidiqi amekumbusha kuwa mapinduzi ya Kiislamu ya mwaka 1979 yaliyoongozwa na Imam Khomeini (M.A) hapa nchini Iran yalikuwa na lengo la kumkomboa kila mpenda haki duniani. Akifafanua zaidi shaksia ya Imam Khomeini (M.A), Hujjatul-Islam Hassan Sidiqi amesema kuwa muasisi huyo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran aliweza kuchora msitari wa kupambanua kati ya mabeberu na wapenda haki. Amesema Waislamu wanayo mengi ya kujifunza kutokana na harakati za ukombozi za Imam Ruhullah Khomeini.
803199
captcha