IQNA

UNICEF: Wazayuni wamezidisha mashambulizi dhidi ya watoto Palestina

16:13 - June 13, 2011
Habari ID: 2137624
Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa UNICEF umetoa ripoti ukisema kuwa Wazayuni wamezidisha mashambulizi dhidi ya watoto wadogo wa Kipalestina katika miezi miwili ya hivi karibuni.
Kituo cha Palestine Info kimerpoti kuwa, katika ripoti hiyo UNICEF imetangaza kwamba askari wa utawala ghasibu wa Israel wameua watoto 10 wa Kipalestina na kujeruhi wengine 117 katika kipindi cha miezi ya Machi na Aprili.
Ripoti hiyo mesisitiza kuwa mashambulizi ya askari wa utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya watoto wadogo wa Palestina yameongezeka maradufu katika miezi hiyo miwili.
Imesema kuwa asilimia 44 ya mauaji hayo yamefanyika katika Quds Tukufu.
Shirika la UNICEF limeitaka jamii ya kimataifa kufanya uchunguzi kuhusu mauaji yanayofanywa na Israel dhidi ya watoto wa Palestina na kuwafikisha mahakamani wahusika. 807967
captcha