IQNA

Jakarta ni mwenyeji wa Kongamano la Kimataifa la Habari

16:31 - June 15, 2011
Habari ID: 2138687
Serikali ya Indonesia kwa ushirikiano na Jumuiya ya Kimataifa ya Kiislamu yenye makao yake Makka inapanga kuandaa Kongamano la Kimataifa la Habari mjini Jakarta mwezi Septemba.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Masuala ya Kidini, Bahrul Hayat amesema kuwa nafasi ya vyombo vya habari katika zama hizi za utandawazi ni muhimu hasa katika Ulimwengu wa Kiislamu.
Amesema kongamano hilo ni kuhusu vyombo vya habari na teknolojia ya mawasiliano katika ulimwengu wa Kiislamu. Aidha linakusudia kutafuta suluhisho kwa nchi za Kiislamu ili ziweze kunufaika na teknolojia ya mawasiliano. Ameongeza kuwa kunapaswa kutafuta mbinu zitakazoziwezesha nchi masikini za Kiislamu kupata faida ya maendeleo ya teknolojia ya mawasiliano.
808657
captcha