Shirika la habari la Kuwait KUNA limeripoti kuwa maonyesho hayo yanayosimamiwa na Baraza la Taifa la Utamaduni la Kuwait (NCCAL) yanajumuisha vitabu 366 na nakala 700 za maandishi ya mkono yaliyokusanywa na Dakta Safvet beg Basagic.
Safvet beg Basagic (1870-1934) maarufu kwa jina la Mirza Safvet alikuwa mwandishi wa Kibosnia na baba wa mageuzi ya nchi hiyo. Vilevile alikuwa malenga mashuhuri mwanzoni mwa karne ya 20. Safvet beg Basagic pia ndiye mwasisi wa Jumuiya ya Utamaduni ya Gojrat na alikuwa kiongozi wa Baraza la Bosnia katika mwaka 1910.
Katika kipindi cha uhai wake mwandishi huyo alikusanya majmui ya nakala nadra na zenye thamani kubwa za Kiislamu na vitabu vya kale vinavyohifadhiwa katika maktaba ya Chuo Kikuu cha mji mkuu wa Slovakia, Bratislava. 813533