IQNA

Iran kuanzisha kituo cha tarjumi na tafsiri ya Qur’ani

14:35 - June 29, 2011
Habari ID: 2146522
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran itaanzisha kituo maalumu cha kazi za tarjumi na tafsiri za Qur’ani Tukufu.
Hayo yamesemwa na Hujjatul Islam Sayyid Ali Akbar Husseini mkuu wa kitengo cha tarjumi na tafsiri katika Taasisi ya Utamaduni na Mafunzo ya Qur’ani.
Kituo hicho kitakuwa na jukumu la kuwakusanya pamoja wataalamu wa tarjumi ya Qur’ani nchini na kuwasilisha maelezo ya kiufundi.
Amesema taasisi hiyo tayari inajishughulisha na kazi za tarjumi na tafsiri. Ameongeza kuwa utafiti unafanyika kuhusu mahitajio ya wanafunzi katika viwango mbalimbali.
816816
captcha