IQNA

Waislamu wa Czech watayarisha mashtaka dhidi ya mwanasiasa aliyevunjia heshima Uislamu

17:15 - July 09, 2011
Habari ID: 2151347
Wawakilishi wa jumuiya za Kiislamu nchini Czech wamekosoa vikali kitendo cha Waziri Mkuu wa zamani wa nchi hiyo Miloš Zeman cha kuvunjia heshima Uislamu na Waislamu na wametayarisha mashtaka dhidi ya mwanasiasa huyo.
Miloš Zeman hivi karibuni aliandika makala katika kituo cha mtandano wa intaneti cha Prvnizrpavy.com akidai kuwa "Uislamu ni dini inayoeneza chuki". Matamshi hayo yamekabiliwa na malalamiko makali ya jumuiya na taasisi za Kiislamu cha Czech.
Zeman amesema katika makala hiyo kwamba: "Vita vya karne ya 21 ni vita kati ya ustaarabu wa Marekani kama dini ya upendo, na ustaarabu wa Kiislamu ambayo ni dini ya chuki, na hapana budi kuchagua moja kati ya staarabu hizo mbili!".
Wawakilishi wa jumuiya za Kiislamu za Czech wametayarisha mashtaka dhidi ya mwanasiasa huyo wakimtuhumu kwa kufanya uchochezi dhidi ya Uislamu na Wislamu.
822402
captcha