IQNA

Indonesia kuchunguza uwezekano wa kufungua kituo cha mazungumzo kati ya tamaduni

18:34 - July 13, 2011
Habari ID: 2154229
Mkuu wa mkoa wa Sumatra Kaskazini nchini Indonesia Rahmati Muhammad amesema kuwa mkoa huo umeanza mashauriano ya awali na Misri juu ya uwezekano wa kuanzisha Kituo cha Kiislamu cha Mazungumzo kati ya Staarabu na Tamaduni Mbalimbali katika mkoa huo.
Rahmati Muhamamd ambaye amekutana na kufanya mazungumzo na balozi wa Misri nchini Indonesia amekitaka Chuo Kikuu cha al Azhar kuunga mkono suala la kuanzishwa Kituo cha Mazungumzo kati ya Tamaduni Mbalimbali katika mji huo.
Lengo la kuasisiwa kituo hicho limetajwa kuwa ni kuweka wazi sura halisi ya Uislamu wenye misimamo ya wastani na kukifanya kituo cha mazungumzo katika eneo la Asia na Pacific.
Kwa upande wake balozi wa Misri mjini Jakarta amesema al Azhar imeanza harakati za kuanzisha mazungumzo kati ya wafuasi wa dini na tamaduni tofauti duniani. Ameongeza kuwa atawasilisha ombi hilo kwa Sheikh wa al Azhar Ahmad al Tayyib. 825258

captcha