IQNA

Mashindano ya Qur'ani ya al-Fujairah mwezi wa Ramadhani

18:38 - July 25, 2011
Habari ID: 2159808
Mashindano ya 5 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu yajulikanayo kama 'Zawadi ya Al Fujairah ya Qur'ani Tukufu' yatafanyika mjini Fujairah katika Umoja wa Falme za Kiarabu katika mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Mkuu wa kamati andalizi ya mashindnao hayo Farhan al Ka'abi amesema mashindano hayo yatakuwa katika kitengo cha hifdhi na yatamalizika tarehe 20 mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Amesema washindi watatunukiwa zawadi katika sherehe za kufunga mashindano.
Amesema pembizoni mwa mashindano hayo kutakuwa na shughuli kadhaa kama vile: 'Ramadhani Inahitaji Watu Wapya'. Mpango huo unalenga kuiarifisha dini tukufu ya Kiislamu kwa wasiokuwa Waislamu.
Aidha kutakuwa na mpango wa kuwaenzi wanafunzi na mahufadh wa Qur'ani katika vyuo mbalimbali vya Imarati katika fremu ya kauli mbiu ya "Qur'ani inaposomwa, Umma wa Kiislamu Unastawi".
831061
captcha