IQNA

Mashindano ya 5 ya kitaifa ya hifdhi ya Qur'ani yafanyika Guinea Conakry

15:22 - August 02, 2011
Habari ID: 2164105
Mashindano ya hifdhi ya Qur'ani Tukufu makhsusi kwa ajili ya vijana na mabarobaro yalifanyika Jumapili iliyopita katika mji wa Conakry nchini Guinea.
Mashindano hayo ambayo yamesimamiwa na Taasisi ya Imam Malik yamewashirikisha wasomaji 30 walioshinda katika duru za awali.
Lengo la mashindano hayo limetajwa kuwa ni kuwahamasisha vijana na mabarobaro kusoma na kuhifadhi Qur'ani Tukufu na kupata wasomaji bora watakaowakilisha Guinea Conakry katika mashindano ya kimataifa ya kuhifadhi Qur'ani katika nchi za Kiislamu.
Mashindano hayo yamefanyika katika vitengo vitatu vya vijana wenye umri wa zaidi ya miaka 18, vijana wa chini ya umri wa miaka 18 na vijana wenye chini ya umri wa miaka 10. 835767

captcha