Hujjatul Islam Walmuslimin Sayyid Tayyib Hussaini amesema kuwa Baraza na Mawasiliano la Vyuo vya Kidini limeunda kamati inayoshirikisha vyuo vya kidini katika Maonyesho ya 19 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Tehran. Ameongeza kuwa taasisi 132 za vyuo vya kidini zilitangaza kuwa ziko tayari kushiriki katika maonyesho hayo lakini kutokana na nafasi ndogo ni taasisi 58 tu ndizo zilizokubaliwa na zimepewa vibanda 20. Ameongeza kuwa vibanda vya taasisi hizo pia vinajumuisha vitengo vya tasnifu za taaluma ya Qur'ani, watoto na kitengo cha Haram ya Bibi Maasuma AS.
Sayyid Tayyib Hussaini amesema kuwa miongoni mwa ajenda za kitengo cha vyuo vya kidini katika Maonyesho ya 19 ya Kimataifa ya Qur'ani mjini Tehran ni vikao vya kukosoa na kujadili filamu za kidini na zenye maudhui ya Qur'ani Tukufu. 835546