IQNA

Nchi 20 zashiriki katika Maonyesho ya Kimataifa ya Qur’ani Tehran

1:31 - August 03, 2011
Habari ID: 2164224
Maonyesho ya 19 ya Kimataifa ya Qur’ani ya Tehran ni mwenyeji wa wachapishaji na watafiti wa Qur’ani kutoka nchi 20 duniani.
Kwa mujibu wa mkuu wa kitengo cha kimataifa katika Shirika la Utamaduni na Mahusiano ya Kiislamu ICRO, watafiti, watarjumi na wachapishaji 23 kutoka nchi 20 duniani wanashiriki katika maonyesho ya mwaka huu. Nchi zinazoshiriki ni pamoja na Ujerumani, Indonesia, Malaysia, India na Ufilipino.
Ameongeza kuwa kitengo hicho cha kimataifa kitafunguliwa rasmi tarehe 9 wezi mtukufu wa Ramadhani katika hafla itakayohudhuriwa na Waziri wa Utamaduni na Miongozo ya Kiislamu pamoja na mkuu wa ICRO.
Maonyesho ya Kimataifa ya Qur’ani ya Tehran yanafanyika katika Uwanja wa Sala wa Imam Khomeini RA hadi tarehe 25 ya mwezi mtukufu wa Ramadhani. 835764
captcha