IQNA

Mashindano ya Qur'ani ya wanafunzi yafanyika Ghana

14:26 - August 07, 2011
Habari ID: 2166380
Awamu ya pili ya mashindano ya Qur'ani ya wanafunzi yamefanyika katika eneo la Ashanti nchini Ghana katika siku za awali za mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Mashindano hayo yameandaliwa na Kituo cha Kimataifa cha Tabligi, na Maktaba ya Imam Khomeini RA kwa ushirikiano na Kituo cha Utamaduni cha Iran mjini Accra, Ghana.
Akizungumza mbele ya washiriki, Kiongozi wa Kishia katika eneo hilo Hujjatul Islam Ali Adam amewapongeza kwa mnasaba wa kuanza mwezi mtukufu wa Ramadhani na akazungumzia umuhimu wa Qur'ani Tukufu.
Ametoa wito kwa Waislamu kuandaa vikao zaidi vya Qur'ani, tafsiri, qiraa na hifdhi katika mwezi mtukufu wa Ramadhani.
837895
captcha