Tarjumi zilizoarifishwa ni za lugha za Kiswahili, Kiingereza, Kijerumani, Kikurdi na Kituruki.
Miongoni mwa tarjumi za Qur'ani kwa lugha ya Kiingereza zilizoarifishwa katika chumba hicho ni ile ya Muhammad Hamid Shakir yenye kurasa 1310. Tarjumi hiyo ya Kiingereza pia ina tarjumi ya Qur'ani kwa lugha ya Kifarsi iliyoandikwa na marehemi Mahdi Ilahi Qamshei.
Tarjumi nyingine za Qur'ani kwa lugha ya Kiingereza zilizoarifishwa ni pamoja na tarjumi za Abdullah Yusuf Ali, Akbar Iranpanah, Sayyid Aliqoli Qarai na Maasuma Yazdan Panah.
Tarjumi ya Qur'ani kwa lugha ya Kiswahili iliyoarifishwa katika kibanda hicho imeandikwa na Ustadh Ali Juma Mayunga na imechapishwa na Taasisi ya uchapishaji ya Ansariyan ya Qum nchini Iran katika kurasa 1588. 838230