IQNA

Kikao cha Mbinu ya Tafsiri ya Ahlul Bayt AS

14:21 - August 08, 2011
Habari ID: 2167161
Kikao cha ‘Mbinu ya Ahul Bayt AS katika kutafsiri Qur’ani’ kinafanyika Jumatatu hii katika Maonyesho ya Kimataifa ya Qur’ani Tehran.
Kikao hicho kinatazamiwa kuanza saa tatu na nusu hadi saa tano usiku,
Kikao hicho kitajumuisha hotuba ya Hujjatul Islam Dashti na katibu wa kikao Hujjatul Islam Sayyed Ali Sadat Fakhr.
Hiki kitakuwa kikao cha nne katika mfululizo wa vikao vilivyoandaliwa na kitengo cha utafiti katika maonyesho hayo.
Vikao vya kwanza vitatu vilihusu, ‘Qur’ani na Utamaduni wa Wakati’, ‘Msingi wa Kufahamu Hadithi za Tafsiri Katika Al Mizan’ na ‘Nafasi ya Hadithi katika Tafsiri ya Qur’ani’.
Kitengo cha utafiti katika maonyesho ya Qur’ani ya Tehran pia kimeandaa warsha mbalimbali kuhusu Qur’ani Tukufu. 838943


captcha