IQNA

Jarida la Kwanza la Kiislamu lachapishwa Bolivia

13:01 - August 08, 2011
Habari ID: 2167174
Jarida la kwanza kabisa la Kiislamu limechapishwa nchini Bolivia. Jarida hilo lijulikanalo kwa jina la “La Apertura” limechapishwa na Waislamu katika Kituo cha Kiislamu cha Bolivia.
Vijana Waislamu na wasiokuwa Waislamu nchini Bolivia wamehusika katika uchapishaji wa jarida hilo ambalo limezinduliwa kwa munasaba wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Toleo la kwanza la jarida hilo lina maudhui kama vile ‘Simon Bolivar na Qur’ani’, ‘Siku ya Uhuru Bolivia’, ‘Kufahamu Mwezi wa Ramadhani’, ‘Waislamu wa Bolivia Mwezi wa Ramadhani’, ‘Uhuru wa Wanawake kwa Mtazamo wa Uislamu’ na ‘Ugaidi kwa Mtazamo wa Uislamu’.
Mhariri Mkuu wa Jarida hilo ni mwanamke wa Kishia ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Bolivia. Amesema toleo la pili litachapishwa kwa mnasaba wa Siku ya Kimataifa ya Quds ambayo huadhimishwa Ijumaa ya mwisho ya mwezi mtukufu wa Ramadhani.
838177

captcha