Vikao vya kufarijika na Qur'ani ambavyo tokea mwanzoni mwa mwezi huu wa Ramadhani vimekuwa vikifanyika katika Haram mbili za Imam Hussein na Hadhrat Abbas (as) huko katika mji mtakatifu wa Karbala viliendelea hapo jana Jumapili ambapo Ahmad Nuina, msomaji mashuhuri wa Qur'ani wa Misri alishiriki.