Kwa mujibu wa waandaaji wa mashindano hayo, yamepangwa kufanyika katika makundi matatu ya hifdhi na tafsiri ya sura 30, 20 na 10 za mwisho za Qur'ani Tukufu. Mashindano hayo yatafanyika bila kuzingatia umri wa washiriki na washindi kutangazwa baadaye alasiri siku hiyohiyo ya mashindano.
Muungano huo wa Waislamu pia unatekeleza ratiba maalumu za hotuba katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani ambapo wanazuoni wa jimbo hilo wanazungumzia masuala mbalimbali yanayohusiana na ulimwengu wa Kiislamu. 840673