IQNA

Nchi 99 katika mashindano ya kimataifa ya Qur'ani Misri

14:18 - August 14, 2011
Habari ID: 2170320
Wawakilishi wa nchi 99 za Kiarabu na Kiislamu watashiriki katika mashindano ya kimataifa ya Qur'ani ya Misri yatakayoanza tarehe 18 mwezi mtukufu wa Ramadhani mjini Cairo.
Waziri wa Waqfu na Masuala ya Kiislamu wa Misri Abdulfadhil Alfusi amesema kuwa mashindano hayo yatakuwa katika vitengo vya kuhifadhi Qur’ani kamili, tajweed, tafsiri ya juzuu moja ya Qur’ani, kuhifadhi juzuu 20 na tajuwidi, kuhifadhi juzuu 10 na tajuwidi na kuhifadhi juzuu tano na tajuwidi.
Ameongeza kuwa mashindano ya mwaka huu pia yana kitengo maalumu cha nchi za wasio zungumza lugha ya Kiarabu ambao watashindana kuhifadhi juzuu sita za Qur’ani Tukufu.
Majaji watakaosimamia mashindano hayo ni kutoka Misri, Saudi Arabia, Bahrain, Senegal, Syria, Algeria na Oman.
841964
captcha