IQNA

Bunge la Iraq lapiga marufuku filamu ya al-Hassan na al-Hussein

15:20 - August 15, 2011
Habari ID: 2170861
Wabunge wa Iraq siku ya Jumamosi walipiga marufuku uonyeshwaji wa filamu ya al-Hassan wal Hussein (as) katika televiseni za satalaiti za nchi hiyo.
Akizungumzia suala hilo bungeni, Usama an-Nujaifi, Spika wa Bunge hilo ameitaka kamisheni inayoshughulikia masuala ya vyombo vya habari na mawasiliano ya bunge hilo kutoa tangazo la kupiga marufuku filamu hiyo inayopotosha ukweli wa kihistoria kwenye televisheni za Iraq.
Kikao hicho cha bunge kilifanyika kutokana na ombi la baadhi ya wabunge, Jumuiya ya Wanazuoni wa Kishia na Kisuni pamoja na mamarja' wa Iraq kwa lengo la kuzuia filamu hiyo isije ikawasha moto wa fitina za kimadhehebu nchini humo. 842877
captcha