Wahanga hao kupitia mawakili wao wamesema kuwa Papa pamoja na waitifaki wake walishindwa kukomesha visa vya ulawiti vilivyokuwa vikifanywa na makasisi na hata wakati mwingine Vatican imekuwa ikiwakingia kifua pamoja na kuwafunika makasisi walawiti. Wahanga hao wamesema kwamba kwa mujibu wa sheria za kimataifa, vitendo hivyo viovu ni jinai dhidi ya binadamu hususan vinapotendewa mtu bila hiari yake. Vatican imepuuzilia mbali wito huo na kuutaja kuwa njia duni ya kujipatia umashuhuri.
861173