IQNA

ICC yatakiwa kumchunguza Papa Benedict kuhusu jinai dhidi ya binaadamu

18:37 - September 14, 2011
Habari ID: 2187480
Wanaume waliolawitiwa na makasisi wa kanisa Katoliki nchini Uholanzi wameitaka Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC ianzishe uchunguzi dhidi ya kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Benedict wa 16 pamoja na maafisa wengine 3 wa ngazi za juu wa Vatican.
Wahanga hao kupitia mawakili wao wamesema kuwa Papa pamoja na waitifaki wake walishindwa kukomesha visa vya ulawiti vilivyokuwa vikifanywa na makasisi na hata wakati mwingine Vatican imekuwa ikiwakingia kifua pamoja na kuwafunika makasisi walawiti. Wahanga hao wamesema kwamba kwa mujibu wa sheria za kimataifa, vitendo hivyo viovu ni jinai dhidi ya binadamu hususan vinapotendewa mtu bila hiari yake. Vatican imepuuzilia mbali wito huo na kuutaja kuwa njia duni ya kujipatia umashuhuri.
861173
captcha