IQNA

Kamati maalumu ya kufuatilia faili la Imam Musa Sadr Libya yabuniwa

15:39 - October 31, 2011
Habari ID: 2215200
Mahmoud Jibril, mkuu aliyestaafu hivi karibuni wa Kamati ya Utendaji ya Baraza la Mpito la Libya alisema jana usiku mbele ya waandishi habari kwamba nchi hiyo imebuni kamati maalumu ya kufuatilia faili la kutekwa nyara Imam Musa Sadr na wenzake wawili na utawala wa dikteta Mummar Qaddafi aliyeuawa hivi karibuni.
Akizungumza mbele ya waandishi habari katika mji wa Tripoli, Jibril amesema kuwa kila kamati ya kigeni inayojishughulisha na masuala tofauti nchini Libya itapasa kutekeleza majukumu yake chini ya usimamizi wa Baraza la Mpito ili kulinda maslahi ya kitaifa ya nchi hiyo.
Amesema baraza hilo linatilia maanani masuala muhimu ya nchi hiyo likiwemo faili la Imam Musa Sadr na kuongeza kuwa suala hilo linashughulikiwa na kamati maalumu ambayo imebuniwa na baraza hilo la mpito.
Amesema kufikia sasa amezungumza mara mbili kwa njia ya simu na Najib Miqati, Waziri Mkuu wa Lebanon na kumfahamisha juhudi ambazo zinafanyika kwa ajili ya kushughulikia faili hilo muhimu. Ameongeza kuwa kutafutiwa ufumbuzi suala hilo kutakuwa na maslahi kwa nchi zote mbili.
Jibril amesema suala hilo linapasa kutatuliwa haraka iwezekanavyo ili kuondoa vizuizi vinavyozuia kuimarishwa uhusiano wa nchi mbili hizo muhimu za Kiarabu. 890386
captcha