IQNA

Waziri wa Wakfu wa Misri alalamikia huduma duni za Saudia kwa mahujaji

17:59 - November 09, 2011
Habari ID: 2220008
Waziri wa Wakfu na Masuala ya Kiislamu wa Misri Muhammad Abdulfadhil ameelezea kutoridhishwa na huduma zinazotolewa na Saudi Arabia kwa mahujaji wa Kimisri.
Abdulfadhil amesema, mahujaji wa Misri waliokwenda kutekeleza ibada ya hija nchini Saudi Arabia wamekutana na mashaka mengi.
Ameongeza kuwa mahujaji wa Misri wamebanwa mno na kukutana na mashaka mengi hususan katika uwanja wa Arafa, Mina na Muzdalifa.
Amesema kuwa nafasi iliyotolewa na serikali ya Saudia kwa mahujaji wa Misri ilikuwa ndogo sana na kwamba tokea sasa msafara wa hija wa mahujaji wa nchi hiyo utasimamiwa na taasisi moja ili kuepusha matatizo yaliyojitokeza mwaka huu. 895475


captcha